Mwenyezi Mungu kwa mapenzi yake makubwa kwa mwanadamu, amemwekea kiumbe huyo njia nyingi rahisi za kuweza kuishi kwa njia salama na kwa manufaa makubwa hapa duniani. Licha ya kwamba mwanadamu ni mwingi wa kukosea, lakini Mwenyezi Mungu kwa mapenzi Yake ametuwekea wazi mlango wa maghufira na kusamehewa madhambi yetu kila sekunde na wakati wowote ule. Lakini pia ili tuweze kuishi kwa raha na utulivu hapa duniani, Mwenyezi Mungu ametuwekea njia nyingi za kufuata ikiwemo kuomba maghfira kwa wingi ili tuweze kupata manufaa ya hapa hapa duniani ya kijamii, kiuchumi, kimaisha n.k, kabla ya manufaa makubwa zaidi ya huko Akhera. Audio hii hapa chini inagusia kidogo suala hilo.

(Visited 233 times, 1 visits today)
One thought on “Manufaa ya duniani ya istighfar”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!