Sahaba wakiratili, tudiriki Shekhe Ali

Wanahiliki rijali, katukhadaa kufari.

*****

Alii akisikia, sauti kumnadia

Akizinga khuyulia, kudiriki askari.

*****

Akimzinga jawadi, yukinga kama asadi

Akiwegama anidi, kwa sefu dhu ‘lFiqari.

*****

Akiwa kuwadhiisha, adhuhuri hata isha

Na mauti kuwegesha, wakivunda makufari.

*****

Wale waliosalia, mambo yakiwatatia

Waliwele kukimbia, qaumu ya ‘lKhatiri.

*****

Kwao walipowasili, wakidhania qitali

Sahaba na Shekhe Ali, walikwisha kudhihiri.

*****

Pakizuka na mayowe, pasi mjua mwenziwe

Hata mtu na mwanawe, wasijuane khabari.

*****

Wakishika malaina, wao kwa wao kuwana

Wasiwe na kujuana, isha hata ufajiri.

*****

Usiku kupambazuka, walitoza mushirika

Wawene watu kanguka, qaumu ya makufari.

(Visited 212 times, 1 visits today)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!